Filamu ya Yesu nchini Tanzania

Filamu ya Yesu katika lugha ya mbalimbali hapa nchini Tanzania.

Filamu ya Yesu nchini Tanzania inaweza kupatikana katika lugha zetu za kienyeji kama Kiswahili, Kisukuma, Kigogo, Kimasai, Kihaya, Kimaasai, Kimakonde, Kimakua, Kinyakyusa, Kinyamwezi, Kilughuru, Kinyia, na Kiyao.

Filamu hii ya Yesu inafaa ndani ya hadithi kubwa ya mila ya Kikristo ya Yudeo. Kusudi la kila kitu tangu uumbaji umekuwa ukionyesha maisha ya Yesu. Uumbaji wote unazungumza juu ya ukuu wa Mungu. Kama Mungu alivyoumba mwanaume na mwanamke aliwakusudia waishi kwa amani na yeye milele. Lakini kwa sababu ya kutotii kwao wanadamu walijitenga na Mungu.

Lakini Mungu bado alikuwa akipenda wanadamu kwa hivyo katika maandiko yote Mungu hufunua mpango wake wa kuokoa ulimwengu.

Filamu ya Yesu katika Lugha ya Kiswahili.

Filamu hii ni katika Lugha ya Kiswahili lugha ambayo ni maarufu sana nchini Tanzania

Tembelea Tovuti yetu ya Kiswahili

Filamu ya Yesu katika Lugha ya Kisukuma

Filamu hii ni katika Lugha ya Kisukuma.

Kisukuma ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania inayozungumzwa na Wasukuma. Mwaka wa 2013 idadi ya wasemaji wa Kisukuma imehesabiwa kuwa watu 7,300,000.
Hii lugha inazungumzwa katika maeneo ya Shinyanga, Geita, na Mwanza. 

Soma Zaidi

Filamu ya Yesu katika Lugha ya Kigogo

Filamu hii ni katika Lugha ya Kigogo.

Hii lugha inazungumzwa katika maeneo ya Dodoma hapa nchini Tanzania

Tembelea Tovuti yetu ya Kigogo

Filamu ya Yesu katika Lugha ya Kihaya

Filamu hii ni katika Lugha ya Kihaya.

Hii lugha yaitwa pia Ekihaya, Luhaya, Oruhaya, ama pia Ruhaya. Mwaka wa 2013 idadi ya wasemaji wa Kihaya imehesabiwa kuwa watu 1,740,000.

Hii lugha inazungumzwa katika maeneo ya Kagera   nchini Tanzania

Lugha hii ina vilugha vingine kama Bumbira, Edangabo, Ganda-Kiaka, Hamba, Hangiro (Ihangiro), Kyamutwara (Kiamutwara, Kjamtwara), Mwani, Nyakisisa, Yoza, Ziba (Ekiziba, Kisiba, Kiziba, Luziba, Naziba, Ruziba, Siba), Bugabo (Bugabu), Bukara, Hanja (Kianja, Kihanja, Kjanja), Missenyi (Misenyi), Nabuddu.

Tembelea Tovuti yetu ya Kihaya

Filamu ya Yesu katika Lugha ya Kilughuru

Filamu hii ni katika Lugha ya Kiluguru.

Kiluguru ni lugha ya Kibantu inayozungumzwa na Waluguru nchini Tanzania.

Mwaka wa 2001 idadi ya wasemaji wa Kiluguru imehesabiwa kuwa watu 692,000. Lugha hii huzungumzwa hasa na Waluguru wanaopatikana katika mkoa wa Morogoro ambao ni wazawa. Sehemu maarufu kwa kuzungumzwa lugha hii ni: Matombo (inayojumuisha Tawa, Kibogwa, Milawilila, Uponda, Kitungwa, Konde, Kiswira), maeneo mengine ni tarafa ya Mgea.

Tembelea Tovuti yetu ya Kiluguru

Filamu ya Yesu katika Lugha ya Kimaasai

Filamu hii ni katika Lugha ya Kimaasai lugha ambayo ni maarufu sana nchini Tanzania.

Filamu ya Yesu katika Lugha ya Kimakonde

Filamu hii ni katika Lugha ya Kimakonde

Kimakonde ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania na Msumbiji inayozungumzwa na Wamakonde. Mwaka wa 2013 idadi ya wasemaji wa Kimakonde nchini Tanzania imehesabiwa kuwa watu 1,320,000.
Hii lugha inazungumzwa katika maeneo ya Mtwara,wilaya ya Tandahimba, na Newala hapa nchini Tanzania

Tembelea Tovuti yetu ya Kimakonde

Filamu ya Yesu katika Lugha ya Kimakua

Filamu hii ni katika Lugha ya Kimakua.

Filamu ya Yesu katika Lugha ya Kinyakyusa

Filamu hii ni katika Lugha ya Kinyakyusa.

Kinyakyusa ama KiNyakyusa-Ngonde ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania inayozungumzwa na Wanyakyusa. Mwaka wa 2013 idadi ya wasemaji wa lugha hii wamehesabiwa kuwa watu wapatao 1,080,000.

Hii lugha inazungumzwa katika maeneo ya Mbeya na Njombe.

Vilugha vyake ni kama vile Nyakyusa (Nyekyosa), Kukwe (Lungulu, Ngumba), Mwamba (Cisociri, Sokelo, Sokile), Ngonde (IkyaNgonde, Konde), Selya (Kaaselya, Salya, Seria), na Sukwa.

Tembelea Tovuti yetu ya Kinyakyusa

Filamu ya Yesu katika Lugha ya Kinyamwezi

Filamu hii ni katika Lugha ya Kinyamwezi.

Filamu ya Yesu katika Lugha ya Kiyao

Filamu hii ni katika Lugha ya Kiyao.

×

Hello!

Click one of our contacts below to chat on WhatsApp

× How can I help you?