Filamu ya Yesu katika lugha ya mbalimbali hapa nchini Tanzania.
Filamu ya Yesu nchini Tanzania inaweza kupatikana katika lugha zetu za kienyeji kama Kiswahili, Kisukuma, Kigogo, Kimasai, Kihaya, Kimaasai, Kimakonde, Kimakua, Kinyakyusa, Kinyamwezi, Kilughuru, Kinyia, na Kiyao.
Filamu hii ya Yesu inafaa ndani ya hadithi kubwa ya mila ya Kikristo ya Yudeo. Kusudi la kila kitu tangu uumbaji umekuwa ukionyesha maisha ya Yesu. Uumbaji wote unazungumza juu ya ukuu wa Mungu. Kama Mungu alivyoumba mwanaume na mwanamke aliwakusudia waishi kwa amani na yeye milele. Lakini kwa sababu ya kutotii kwao wanadamu walijitenga na Mungu.
Lakini Mungu bado alikuwa akipenda wanadamu kwa hivyo katika maandiko yote Mungu hufunua mpango wake wa kuokoa ulimwengu.
Filamu ya Yesu katika Lugha ya Kiswahili.
Filamu hii ni katika Lugha ya Kiswahili lugha ambayo ni maarufu sana nchini Tanzania
Kisukuma ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania inayozungumzwa na Wasukuma. Mwaka wa 2013 idadi ya wasemaji wa Kisukuma imehesabiwa kuwa watu 7,300,000. Hii lugha inazungumzwa katika maeneo ya Shinyanga, Geita, na Mwanza.
Kiluguru ni lugha ya Kibantu inayozungumzwa na Waluguru nchini Tanzania.
Mwaka wa 2001 idadi ya wasemaji wa Kiluguru imehesabiwa kuwa watu 692,000. Lugha hii huzungumzwa hasa na Waluguru wanaopatikana katika mkoa wa Morogoro ambao ni wazawa. Sehemu maarufu kwa kuzungumzwa lugha hii ni: Matombo (inayojumuisha Tawa, Kibogwa, Milawilila, Uponda, Kitungwa, Konde, Kiswira), maeneo mengine ni tarafa ya Mgea.
Filamu hii ni katika Lugha ya Kimaasai lugha ambayo ni maarufu sana nchini Tanzania.
Filamu ya Yesu katika Lugha ya Kimakonde
Filamu hii ni katika Lugha ya Kimakonde
Kimakonde ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania na Msumbiji inayozungumzwa na Wamakonde. Mwaka wa 2013 idadi ya wasemaji wa Kimakonde nchini Tanzania imehesabiwa kuwa watu 1,320,000. Hii lugha inazungumzwa katika maeneo ya Mtwara,wilaya ya Tandahimba, na Newala hapa nchini Tanzania
Kinyakyusa ama KiNyakyusa-Ngonde ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania inayozungumzwa na Wanyakyusa. Mwaka wa 2013 idadi ya wasemaji wa lugha hii wamehesabiwa kuwa watu wapatao 1,080,000.
Hii lugha inazungumzwa katika maeneo ya Mbeya na Njombe.
Vilugha vyake ni kama vile Nyakyusa (Nyekyosa), Kukwe (Lungulu, Ngumba), Mwamba (Cisociri, Sokelo, Sokile), Ngonde (IkyaNgonde, Konde), Selya (Kaaselya, Salya, Seria), na Sukwa.